Kesi ya kusambaza picha za ngono kupitia mtandao wa Instagram inayomkabili msanii Wema Sepetu imefikisha siku 42, huku upelelezi ukiwa haujakamilika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Kesi hiyo ilipangwa leo kwa ajili ya kutajwa mbele ya Hakimu Mkazi Maira Kasonde, ambapo Wakili wa Serikali Mosia Kaima amedai upelelezi haujakamilika.