المدة الزمنية 36:54

Salama Na Lady Jaydee Ep 24 | POWERHOUSE Part 1

بواسطة YahStoneTown
111 973 مشاهدة
0
1.2 K
تم نشره في 2020/07/12

#YAHStoneTown #SalamaNa #PodCast SUBSRIBE TO OUR CHANNEL https://bit.ly/YahStoneTownSubs Listen our Podcast on Spotify Link https://spoti.fi/2Uxr6Cm� �� ‪ApplePodcast Link https://apple.co/2Ou1bru� �� GooglePodcast Link https://bit.ly/GooglePodcastSalamaNa Audiomack Link https://bit.ly/YahStoneTownAudioMack ‪YouTube Link http://bit.ly/YoutubeSalamaNa Kwa Judith Wambura Mbibo kuongea anayoyawaza bila ya kupepesa au kutafuta sapoti kabla hajafanya hivyo ndo hulka yake haswa, si wa kukwepeshakwepesha au kung’ata maneno ili yawe malaini zaidi kwa anayeambiwa asijikie vibaya labda. Kwake yeye lilivyo ndo lilivyo, kazi ya kupaka mawingu rangi huwaachia wahusika, yeye yake ni kuhakikisha mawingu yapo, na kwa hilo? Mimi namheshimu sana. Mwanangu mwengine ambaye hii ni mara yetu ya kwanza kukaa chini na kutia story ili wananchi waweze kupata majibu ya baadhi ya maswali waliyokua nayo muda mrefu sana pengine. Na round hii nilihakikisha sichezi mbali naye kama Chama na Mogella, na kwa bahati nzuri muda wake na wangu ukaenda vizuri kabisa kwa sote kuweza kuifanya kazi hii. Ijumaa ya kuamkia Jumamosi ili kuweza kuifanya kazi hii ulikua usiku mfupi sana kwangu. Mawazo yalikua huko tu kwa Jide na kwa kwa watu wengine watatu ambao nlikua na kikao nao. Na Nashkuru Mungu mambo yalienda kama yalivyopangwa. Kuanzia kulelewa na Kaka zake alipokuja Dar es Salaam na kuhakikisha anakua katika maadili mema kwahiyo haikua rahisi kwake kuhakikisha agenda yake ya kutaka kuwa msanii na mara nyengine alikua akichezea kichapo kwasababu tu alikua harudi nyumbani kwa wakati au nyendo zake zilipokua hazieleweki. Baba yake alifariki zamani na Mama yake alifariki 2017 kama nitakua sawasawa. Sikutaka kwenda kwenye details sana juu ya kifo cha Mama yake ila zaidi nilikua nataka tuongelee ubora wake ambao umekua ni kivutio kikubwa kwa wale wanaoanza na ambao tayari washaanza. Kujifunza kwake juu ya ukomavu, uvumilivu, jinsi ya kujibeba. Kutafuta nafasi, kutokata tamaa na kuandika historia. Na kwa hilo alituambia mengi. Kuna issue ya wivu, ndoa, kazi, mahusiano, kipaji na kuwa mwanamke ndani ya kiwanda kichanga ambacho kimezungukwa na wanaume na jinsi ya kupasua milango ya kuziba matabaka ili mambo yaende na historia iandikwe. Vipi aliwezaje ku push hivyo? Na lini haswa alijua ana kipaji chake kikubwa ambacho kinatakiwa kuonekana? Kuna support yoyote aliipata toka nyumbani? Na je baada ya mlango kufunguka, aliwezaje ku maintain hiyo nafasi? Mwaka huu wa 2020 Lady Jay Dee anatimiza miaka ISHIRINI toka ameanza kufanya mziki RASMI. Je hii ndo definition ya MAFANIKIO kwake? Yangu matumaini maongezi yetu yatasaidia sehemu flani na kuongeza jambo kwenye mbio zako za kutaka kuzifuata ndoto zako. Tafadhali enjoy. Love, Salama. Soundtrack Yeah by @MarcoChali /watch/QLnf4BH1euC1f Follow: Twitter: http://twitter.com/YahStoneTown Instagram: http://Instagram.com/YahStoneTown Facebook: http://facebook.com/YahStoneTown

الفئة

عرض المزيد

تعليقات - 197