Hawa ni miongoni mwa viongozi na wanachama wa chama cha ACT Wazalendo kisiwani Pemba, ambao kwa siku za hivi karibuni wamekuwa wakivamiwa majumbani mwao nyakati za usiku na watu wanaosema ni vikosi vya SMZ ambao huwapiga, kuwatesa, kuwadhalilisha na familia zao pamoja na kuwaibia mali zao mbele ya macho ya jeshi la polisi. Hii hapa ni kauli yao.