Simani ni mtoto pekee katika familia yao. Anaishi na mama yake katika kijiji cha Ngirikisande. Maisha yao yamegubikwa na umaskini uliokithiri baada ya baba yake kupotea katika mazingira ya kutatanisha (wakati Simani akiwa mtoto mchanga) alipoenda kuwinda kwenye pori la Mtevyamajini linalohofiwa kuwa na majini yalayo watu.
Simani anafichwa siri hiyo hadi anapokuja kuifahamu akiwa na miaka kumi na mbili. Akiwa amechoshwa na maisha ya kutokuwa na baba na kutaniwa na marafiki zake kijijini hapo, Simani na mbwa wake Boji wanatoroka na kufunga safari ya kwenda kumsaka baba yake kwenye pori la Mtevyamajini, lenye majini hatari.