المدة الزمنية 15:47

OR-TMSMIM ZANZIBAR

بواسطة OR-TMSMIM ZANZIBAR
273 مشاهدة
0
9
تم نشره في 2021/09/02

Taasisi za kifedha zimeshariwa kuunga mkono miradi yenye Tija ya uwekezaji na uzalishaji iliyoibuliwa na Afisi ya Rais Tawala za mikoa Serikali za mitaa na Idara maalum za smz. Akizungumza na uongozi wa Benki ya NMB afisini kwake Vuga Waziri wa nchi Afisi ya Rais TAWALA za mikoa serikali za mitaa na idara maalum za smz Mh Masoud Ali Mohamed amesema utekelezaji wa miradi hiyo kupitia benk ya Huduma Kwa wateja NMB itakuwa na faida Kwa pande zote mbili. Amesema Idara maalum pamoja Tawala mikoa na Serikali za mitaa zitajiongezea kipato na kuweza kujitegemea na kupunguza kutegemea ruzuku kutoka serikali Kuu, ambapo Benki ya NMB itakuwa na uhakika wa kupokea mrejesho kutoka taasisi hizo. Wakiwasilisha miradi hiyo Mkurugenzi mipango Sera na utafiti Afisi Ya Tamisemim Abdalla ISSA Mgongo na Makamanda WA idara maalum za smz wamesema miradi ya maegesho, vituo vya mabasi, masoko, miradi kilimo, UVUVI na huduma za jamii imezingatia mahitaji ya kijamii. Nae Afisa mkuu wateja wakubwa na Serikali Alfred Shao amesema wamepokea mapendekezo yaliyotolewa na kuahidi kushirikiana na Taasisi hizo Kwa lengo la kuleta ufanisi katika upatikanaji wa huduma Bora Kwa wote.

الفئة

عرض المزيد

تعليقات - 0